fbpx
23 Mar
11:48

Mbinu Za Kusoma Wakati Wa Likizo

Mara tu calendar inapoanza mwezi wa kumi, kila mtu anawaza likizo na sikukuu zinazofungamana nazo. Hali ya hewa huwa ni nzuri sehemu nyingi hivyo watu huanza kufikiri jinsi watakavyo tumia likizo zao, sikukuu za Eid, Christmass, Mwakampya na nyenginezo kufurahi na ndugu, jamaa na marafiki wa karibu.

Pamoja na sikukuu zote hizi na muda wa kupumzika, ukiwa mwanafunzi bado inakulazimu kwenda shule, kusoma vitabu, kuingia library kujisomea, kufanya majaribio ya kisanyansi na mambo mengine mengi ya kielimu yanayoweza kukufanya usifurahie wakati wa likizo na sikukuu kwa raha. Hivyo basi ni vizuri sana kutoruhusu msimu huu wa sikukuu kukuharibia mwelekeo wako wa elimu katika kutimiza ndoto zako.

Ondoa vipingamizi.

Vipingamizi au vizuizi huwa vipo kila wakati, lakini kwa msimu huu wa sikukuu huongezeka sana kutokana na muda mwingi unaohitajika kuwa na familia, marafiki na ndugu wa karibu hivyo kutengeneza muda kwa ajili ya masomo huwa ni ngumu sana kipindi hiki.

Na hapa ndio tunasema nidhamu katika elimu ni kitu muhimu sana kwa mwanafunzi kuliko vyote. Inabidi uweze kufurahi na kusherekea muda wako na familia lakini ni muhimu pia kuweka usawa kati ya masomo na muda wa kupumzika.

Dondoo za jinsi ya kusoma wakati wa likizo

Hapa tumekuwekea vitu vichache vinavyoweza kukusaidia kufurahia likizo yako bila kupoteza hamu ya kusoma wakati wa likizo.

  • Weka Mipango ya baadae; jaza calendar yako ukianza na siku ambazo unajua utatakiwa kuwa unasherekea na familia pamoja na marafiki, Kisha angalia siku ambazo unaweza kutenga muda wa kujisomea. kwa mfano siku kama mwaka mpya, unaweza ukatenga siku ya pili yake kwa kujisomea baada ya kuondoa uchovu wa mkesha na maongezi ya hapa na pale siku inayofuata ukafanya ndio ya kujisomea.
  • Beba vitabu vyako; unaweza ukashawishika kuacha kazi za shule shuleni ili kwenda kufurahia likizo na familia yako, lakini ni vizuri kubeba vifaa vyako kwa sababu huwezi kujua ni wakati gani utapata muda ukajisomea
  • Tumia marafiki au familia kama sehemu ya kujifunzia; kuna uwezekano mkubwa wa kukutana na watu wanaoweza kukusaidia kwenye masomo, inaweza kuwa ni wana familia wanaojua unachosoma au marafiki wanaosoma kitu hicho hicho isipokuwa shule tofauti, nufaika na muda unaokaa nao kwa kuwauliza maswali ya hapa na pale.